Suarez ambaye ameanza taratibu maisha yake ya soka Barcelona anachukua dau la pauni 10 milioni kwa mwaka, lakini inadaiwa kuwa atakatwa dau la pauni 3 milioni kama akimng’ata mchezaji wa timu pinzani.
LUIS Suarez itabidi awe mpole tu. Imegundulika kuwa kama akifanya tena ujinga wake wa kung’ata mtu pale Nou Camp basi atalambwa dau kubwa la mshahara wake wa mwaka, hii ni kwa mujibu wa mkataba wake na Barcelona.
Suarez ambaye ameanza taratibu maisha yake ya soka
Barcelona anachukua dau la pauni 10 milioni kwa mwaka, lakini inadaiwa
kuwa atakatwa dau la pauni 3 milioni kama akimng’ata mchezaji wa timu
pinzani.
Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay tayari
amewang’ata wachezaji watatu katika maisha yake ya soka akichezea klabu
za Ajax, Liverpool na timu yake ya taifa ya Uruguay.
Novemba 20, 2010 alimng’ata mchezaji wa PSV, Otman
Bakkal katika pambano la Ligi Kuu ya Uholanzi lililomalizika kwa suluhu
ya bila kufungana. Klabu yake ya Ajax ilimsimamisha mechi mbili na
kumtoza faini.
Kama vile haitoshi, April mwaka jana alimng’ata
mlinzi wa Chelsea, Branislav Ivanovic katika pambano la Ligi Kuu ya
England uwanja wa Anfield. FA ilimfungia mechi 10 za Ligi Kuu ya englad.
June mwaka huu alimalizia Hat trick yake ya
kung’ata wakati alipomng’ata mlinzi wa timu ya taifa ya Italia, Giorgio
Chielini katika pambano la kombe la dunia nchini Brazil. Alifungiwa
kucheza soka kwa miezi minne huku akifungiwa mechi kumi za timu yake ya
taifa ya Uruguay.
Hata hivyo, baada ya uhamisho huo, staa huyo
alikamilisha uhamisho wa pauni 75 milioni kwenda Nou Camp kutoka Anfield
huku akiingia mkataba wa miaka mitano ambayo unamfanya alipwe mshahara
wa pauni 200,000 kwa wiki. Mshahara huo unamfanya awe mchezaji wa nne
kwa kulipwa zaidi katika klabu ya Barcelona nyuma ya Lionel Messi,
Neymar na Andres Iniesta, lakini huenda ukashuka maradufu kama
akiendeleza tabia zake za Ajax na Liverpool.
Mkataba wa Barcelona kwa Suarez ni mkali na
utamuona mchezaji huyo akipoteza kiasi cha asilimia 15 hadi 30 ya
mshahara kama akirudia kung’ata wachezaji wa timu pinzani.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa mabosi wa Barcelona kwa
kiasi kikubwa walishukuru kitendo cha Suarez kumng’ata Chiellini kwa
sababu kwa kiasi kikubwa kiliharakisha mazungumzo kati ya timu yao na
Anfield.
Kitendo hicho kilishusha thamani ya Suarez kwa
kiasi kikubwa na ni timu chache ambazo ziliamua kufukuzia saini yake
mara baada ya kung;ata nchini Brazil.
Kuhakikisha kwamba tukio hilo halitokei tena, hivi
karibuni nyota huyo amekiri kwamba kwa sasa anapata msaada wa matibabu
ya kisaikolojia kuhakikisha kwamba hawezi kufanya tena kitendo hicho
katika siku za karibuni.
No comments:
Post a Comment